Posts

Image
 CHANGAMOTO YA UHABA WA MAJI WATOWEKA SHULENI Moja ya changamoto zinazowakabili wanafunzi wengi wakiwa katika mazingira ya shule zao hapa nchini ni ukosefu wa huduma ya maji safi na salama kwa ajili ya matumizi ya usafi ,kupikia na kunywa. Hali hiyo huwasababishia magonjwa mbalimbali yakiwemo ya kuhara,minyoo na amiba na wakati mwingine hulazimika kutumia muda wa masomo kutafuta huduma ya maji na hata wanapoyafikia yanakuwa si safi na salama. Waumini wa kanisa la Pentekost Galilaya Tanzania lenye makau makuu yake katika mji wa Runzewe limeguswa na adha ya maji inayowakabili wanafunzi wa shule ya sekondari Siloka halmashauri ya wilaya ya Bukombe mkoani Geita baada ya kuvuta huduma ya maji safi na salama hadi shuleni hapo.  Ilikuwa mapema ya February 13,mwaka huu waumini wa kanisa hilo walipokusanyika kwenye shule hiyo na kuchimba mtalo wa kupitisha bomba la maji hadi kuhakikisha maji hayo yanatoka katika shule hiyo. Akizungumziahatua hiyo kwa niaba ya Askofu mkuu wa kanisa hilo...

DKT. BITEKO AZINDUA ZAHANATI YA BUNGONI - ILALA

Image
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko leo tarehe 29 Disemba, 2023 amezindua Zahanati ya Bungoni iliyopo mtaa wa Mafuriko Ilala  jijini Dar es Salaam na kuwataka wananchi kutumia fursa ya  uwepo wa huduma ya zahanati hiyo kutumia huduma badala ya kwenda mbali kufuata huduma za Afya, kwani ni dhamira ya Serikali kusogeza huduma kwa wananchi.  "Niwaombe viongozi wenzangu tuliopewa dhamana na Mhe. Rais kuhakikisha tunawahudumia kwa vitendo wananchi na kuinua hali za wanyonge kwa kuwapatia huduma bora wanazostahili." Alisisitiza Dkt. Biteko Aliwataka wananchi wa Ilala kumpa ushirikiano Mbunge wao kwa vitendo na kumpongeza kwa kazi kubwa aliyofanya ya kuleta Maendeleo kwa wanachi wake, na kuwataka viongozi wengine kuiga mfano wa Mbunge huyo kufanikisha ujenzi wa zahanati hiyo na kukemea wachache wanaojificha kwenye kivuli cha taratibu kuchelewesha maendeleo.  Ujenzi wa zahanati hiyo ulianza mwezi februari mwaka huu, kwa jitihada za wananchi na baadae...